Jumanne, 26 Julai 2016

SHILINGI 1.6BILIONI KUTUMIKA KUFANYA MABORESHO YA TAARIFA KWA WANANCHI .

Tokeo la picha la mussa iyombe
Katibu MKUU TAMISEMI MHANDISI MUSSA IYOMBE


Timothy Marko .
ZAIDI  yashilingi bilioni 1.6 zinatarajiwa Kutumiwa naserikali Katika maboresho ya upatikanaji wa taarifa za wananchi kupitia mfumo wa kiletroniki ili kuiwezesha serikali kuweza kupanga mpango mbalimbali ikiwemo kuwa patia huduma stahiki wananchi. 

Akizungumza na waandishi wa Habari mapema hii leo jijini Dar es salaam Katibu Mkuu Ofisi ya Rais –TAMISEMI Mhandisi Mussa Iyombe amesema kuwa mfumo huo utawezsha kupata taarifa katika ngazi yakitongoji na mtaa .

‘’Mfumo huu unaotumia Data base umeweza kutumika katika nchi za Botswana,Syecelles,Tanzania ,Zanzibar na Mauritus nan chi ambazo zina idadi yazaidi milioni 1 ,Nchi nyingine zinaendelea juhudi za kuboresha mifumo yake kama Tanzania ‘’alisema Katibu Mkuu Mhandisi Mussa Iyombe .

Mhandisi Iyombe alisema kuwa mfumo huo utawezesha kufanya utambuzi wa Raia kwangazi yakitongoji na mtaa na kutunza kumbukumbu za rejista za wakaazi wote nchini .

Alisema Mfumo huo umewahi kutumika katika nchi za ulaya Sweden Norway nanchi Nyinginezo katika ukanda wa bara la ulaya na amerika .

‘’Mfumo huu sio jambo jipya kwa nchi yetu tulikuwa na mfumo huu ambao tulikuwa tunatumia dafutari maalumu la ukaazi kinacho fanyika hivi sasa nimaboresho yataarifa kwa njia ya mfumo wa kiletroniki ‘’Aliongeza Katibu Mkuu Mussa Iyombe .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni