Jumatano, 27 Julai 2016

MPIGA CHAPA WASERIKALI AWATAKA WANANCHI KUHESHIMU VIELELEZO VYA SERIKALI

Tokeo la picha la kassian chibogoyo

Mpiga chapa wa SERIKALI Kassian Chiboyo

Timothy Marko.
Ofisi ya Mpiga Chapa wa Serikali nchini imewataka Wananchi kuheshimu vielezo vya taifa ikiwemo  Bendera ya Taifa ,wimbo wataifa na Nembo ya Taifa .
Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam Mpiga chapa wa ofisi wa ofisi hiyo Kassian Chibogoyo amesema kuwa kwamujibu wa sheria ya bunge ya mwaka 1971 na sheria ya bendera yataifa ya mwaka 1962 na sheria yangao ya taifa Cap .504 ,pamoja sheria ya alama za taifa inamkataza mtu yeyeote kutumia bendera yataifa nangao yataifa kinyume nailivyokusudiwa .
‘’Sheria hizi zinamkataza mtu yeyote kutumia bendera ,nembo yataifa au chochote kinacho fanana na bendera ya taifa na ngao ya taifa kama alama yabiashara au shughuli za kitaluma au kwenye maandiko yanayokusudia Mauzo ‘’Alisema  Kassian Chibogoyo
Mpiga Chapa wa serikali Chibogoyo alisema kuwa mtu yeyote atakaye kaidi anaweza kuhukumiwa kifungo kisichozidi miaka miwili .
Alisema kuwa nikosa la kisheria kutoa lugha ya kashifa au kuandika maneno yenye lengo lakukashifu bendera au nembo ya taifa kwani unaweza kufungwa kifungo kisicho zidi miaka miwili .
‘’msisitizo wa kuheshimu vielezo vya taifa upo katika kanuni ya utumishi wa umma wa mwaka 2009kifungu cha q.20 ambacho kinaonya kuwa bendera ya taifa iliyo tobokatoboka au kupauka au chafu nimarufuku kutumika ‘’Aliongeza chibogoya .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni