Alhamisi, 21 Julai 2016

HRLC:MATUKIO YAUKIKWAJI WA HAKI YAKUISHI YAMEKUWA YA KIONGEZEKA .

Mkurugenzi wa Kituo cha sheria na Haki za binadamu nchini Hellen Kijo


Timothy Marko.
KITUO cha sheria nchini kimesema haki ya kuishi imekuwa ikikiukwa mbele ya vyombo vya dola baada ya vyombo hivyo kujichukulia sheria mkononi hali inayochangia watu mbalimbali kufa wakati wakiwa chini ya vyombo vya dola  .

Akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi wa ripoti ya hali ya Haki za binadamu nchini Mkurugenzi wa Kituo cha sheria na Haki za binadamu nchini Hellen Kijo amesema jumla yawatu 394 walikufa kutokana mauaji yavitendo mateso yavikongwe katika maeneo ya vijijini .

‘’Ongezeko hili la 394 nikubwa ikilinganishwa vifo vilivyotokea mwaka 2015 ambapo vifo 57 viliweza kuripotiwa katika kipindi cha mwaka jana ‘’alisema MkurugenzI wa kituo cha Sheria Hellen Kijo.

Kijo alisema taarifa za jeshi lapolisi zinaonesha kuwa kumekuwa namatukio ya mauaji kwa watu kujichukulia sheria mkononi yamekuwa yakipungua ,hata hivyo katika kipindi chamwaka huu watu 135 waliuwawa kutokana kujichukulia sheria mkononi 
.
Alisema japo taarifa hii haioneshi idadi yawatu waliojeuriwa kutokana kutoka namatukio ya kujichukulia sheria mikononi matukio haya yanaonekana kuwa mengi .

‘’Matukio ya vifo kwa kipindi hiki cha nusu mwaka nipungufu sana ikilinganishwa nakipindi hiki kwa mwaka jana ambapo taarifa zinaonesha vifo vya watu 366 viliweza kuripotiwa ‘’Aliongeza Bi Hellen KIJO .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni