Jumatano, 24 Agosti 2016

TANZANIA NA DRC KUSHIRIKIANA KATIKA UJENZI WABOMBA LA MAFUTA.

Tokeo la picha la bomba la mafuta

picha ya bomba lamafuta



Timothy Marko.
SERIKALI ya Tanzania kwa kushirikiana nanchi ya Kidemokrasia ya watu wa Congo zimeingia makubaliano ya ujenzi wa bomba la Mafuta katika ziwaTanganyka ,ambapo ujenzi wabomba hilo unatarajiwa kuanza mwezi October mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari Mapema hii leo jijini Dar es salaam Waziri wanishati na Madini professa Sospeter Muhongo amesema kuwa ujenzi wa bomba hilo unaotarajiwa kuanza mwezi October mwaka huu unatarajia kuanza katika maeneo ya kabale Uganda nakwenda zaire ukipitia katika ziwa Tanganyika lilopo mpakani mwa nchi hizo mbili .

‘’Mafuta pamoja na gesi yatakayogundulika katika ziwa Tanganyika tunampango wakugawana baina yanchi hizi mbili yani Congo na Tanzania ‘’Alisema Waziri wanishati na Madini sospeter Muhongo .

Profesa Muhongo amesema kuwa kwasasa tayari serikali ya Congo na Tanzania zimekubaliana kampuni ambayo itakayo jihusisha na uchimbaji itaweza kusafirisha mapipa 20,0000 kwasiku .

Kwaupande wake Waziri wanishati wanchini Congo Profesa Aime Ngoi Mukena amesema kuwa ujenzi wa bomba hilo utakao unganisha nchi za Rwanda Uganda na Kongo nimuhimu kwa uchumi wanchi hizo katika kujenga uchumi kupitia sekta hiyo.

Alisema kuwa hatua iliyofikiwa nanchi hizo kuungana katika ujenzi wa bomba hilo la mafuta nagesi unafananishwa kama zawadi kutoka kwa mungu hivyo nivyema nchi hizo kutumia rasmali hiyo ili kujiletea maendeleo ya kiuchumi 
.
‘’Ninayofuraha Kwa Tanzania Uganda Rwanda kuungana katika ujenzi wa bombahili lamafuta ambapo mkutano wa makubaliano ya awali yatafanyika mwezi October mwaka huu ni hatua kubwa kwani hatua hii nizawadi kutoka kwamungu ‘’Alisema Profesa  Aime Ngoi Mukena .

Waziri mukena alisemakuwa hatua hiyo itawezesha kongo kunufaika namafuta kutoka katika ziwa Tanganyika .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni