Msemaji wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Christopher Ole Sendeka akisisitiza jambo katika mkutano na waandishi uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam |
Timothy Marko.
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kimeunga mkono kitendo cha Jeshi la
Polisi kuzuia maandamano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
yanayotarajiwa kufanyika Septemba Mosi mwaka huu kwa kuwa kufanya hivyo kunatokana
na hali ya mazingira ya nchi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Msemaji
wa Chama hicho Christopher Ole Sendeka amesema kuwa Jeshi la Polisi lina
mamlaka ya kuzuia mikutano ya kisiasa kutokana hali ya kimazingira.
‘’Sheria ya Jeshi la Polisi kifungu cha 11 na cha 6 cha jeshi
hilo kinatoa mamlaka ya kutoa zuio la kutokufanyika kwa mikutano ya kisiasa ama
mikutano yoyote kulingana na hali ya kimazingira ya jeshi hilo ‘’Alisema Ole
Sendeka.
Ole Sendeka ameongeza kuwa ni vyema watanzania wakaendelea na
shughuli za kujiletea maendeleo na kuyapuuza maandamano hayo yanayotarajiwa
kufanyika septemba Mosi mwaka huu.
Alisema kuwa chama hicho hakitokubali damu ya watanzania
imwagike kwani wamepewa dhamana ya kulinda amani ya nchi ili iweze kustawi..
‘’uhuru unaotolewa na Vyama vya Siasa kufanya siasa una
kikomo ,Jeshi la Polisi lina wajibu wa kuzuia mikutano endapo itaona mikutano
hiyo ina lengo la kuhatarisha amani ya nchi , jeshi limepewa mamlaka kuzuia
mikutano hiyo ambayo ina viashiria vya uvunjifu wa amani ‘’Aliongeza Ole
Sendeka.
Aliongeza kuwa kitendo cha Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA) kuwasiliana na Jumuiya ya Kimataifa juu ya mwenendo wa siasa nchini kimeleta
sintofahamu kwa jumuiya ya kimataifa juu ya mwenendo wa siasa hapa nchini.
Olesendeka aliongeza kuwa tayari mashirika ya kimataifa na vyombo
vya habari vya kimataifa vimetuma wawakilishi wao kuja kuangalia hali ya kisiasa
hapa nchini.
‘’kumekuwa na mashirika ya kimataifa yakiwemo ya CNN na BBC
yameshatuma wawakilishi wao kuja kuangalia tukio la Septemba 1 na mwenendo wa
sisasa kuhusiana na mandamano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo ‘’Alisisitiza
Ole Sendeka.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni