Jumatano, 20 Julai 2016

ZAIDI YA WATOTO MILIONI 264 DUNIANI WAMEKUWA WAKITUMIKISHWA .

MKURUGENZI WA OFISI YATAKWIMU Dk.Albina Chuwa .




TimothMarko.
MKURUGENZI   wa ofisi ya Takwimu nchini Dk.Albina Chuwa amesema kuwa hali yautumikishwaji wa watoto imekuwa tatizo kubwa duniani ambapo zaidi ya watoto milioni264 duniani kote wamekuwa wakitumikishwa .

Akizungumza katika uzinduzi wa Ripoti ya hali ya utumikishwaji wa watoto ya mwaka huu (Child Labour )mapema hii leo jijini Dar es salaam Mkurugenzi huyo amesema kuwa watoto waliopo kati yaumri wa miaka 5-17 wamekuwa wakitumikishwa. 

‘’Utafiti unaonesha kuwa katika kipindi cha mwaka 2014/15watoto milioni 15wenye umri kati yamiaka mitano hadi kumi nasaba ,ambapo watoto milioni 4.2 sawa na asilimia 28.8 wanatumikishwa katika kazi mbalimbali za kiuchumi.’’Alisema Mkurugenzi wa ofisi Takwimu Dk.Albina chuwa .

Mkurugenzi wa ofisi ya Takwimu Dk.Chuwa alisema kuwa katika Sekta ya kilimo ,Misitu na uvuvi imeendelea kuwa sekta inayo ajiri watoto wengi zaidi kwakiwango cha asilimia 92.1 ya watoto wote wanaojihusisha nashughuli za kiuchumi .

Alisema kuwa Watoto wengi hutumia zaidi ya nusu yamuda wao katika siku katika shughuli za kujihudumia zaidi ikiwemo kujihudumia nausafi huku wasichana wakitumia muda huo katika shughuli za usafi nahuduma zinginezo .

‘’Asilimia 58.8 ya watoto wakiwemo wasichana hutumia muda muda mwingi zaidi katika usafi nashughuli binafsi ikilinganishwa na wavulana ambapo hutumia asilimia 58.3 katika shughuli za kujisomea ‘’.Aliongeza Dk.CHUWA .

Naibu Waziri Ofisi ya waziri Mkuu Sera,Bunge ,Kazi ,Vijana ,ajira nawatu wenye ulemavuDk.Abdallah Possy  amesema kuwa serikali itaendelea kupambana vikali nakupinga utumikishaji wa watoto kwa kuanzisha progaramu ya elimu bure ilikuweza kuhamasisha mahudhurio shuleni .

Alisema kuwa ili kuweza kupunguza ajira za utotoni serikali inawataka kwa wazazi na walezi kutumia vyema fursa katika kuwapeleka watoto shule ilikuondokana natatizo lamimba mashuleni ,na ajira za watoto .

‘’niwaombe Shirika la kazi Duniani ILO Kuendelea kushirikiana na ofisi ya takwimu ilikufanya uchambuzi zaidi wakitalamu ilikupata makadirio yaviwango vya utumikishawaji wa watoto katika ngazi za chini ‘’Aliongeza Dk.Possy.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni