Jumatatu, 18 Julai 2016

SERIKALI KUTOA MUONGOZO WA UTEKELEZAJI WA UMILIKI WAUCHUMI KUPITIA SEKTA YA MAFUTA GESI.

Tokeo la picha la gesi mtwara
MOJA YA MITAMBO YAGESI ILIYOPO MTWARA


Timothy Marko.
SERIKALI imesema itapitia kwa upya mifumo ya kuratibu sekta ya mafuta na gesiasilia nakutoa muongozo wa utekelezaji wa sekta hiyo ilikuweweza kukuza ushiriki wa watazania kunufaika na rasmali hiyo .

Akizungumza na waandishi mapema hii leo jijini Dar es salaam Katibu Mkuu ofisi ya Waziri Mkuu Dk.Hamisi Mwinyimvua amesema kuwa katika kipindi cha Mwezi Mei mwaka jana serikali ilipitisha sera yaushiriki wa watanzania katika sekta ya mafuta nagesi wakati huo huo serikali ilipitisha sheria petroli ambayo inatoa fursa kwa wanachi kushiriki katika kujenga uchumi kupitia sekta hiyo.

‘’Katika kipindi cha mwezi September mwakajana serikali iliagiza kupitia ofisi ya waziri Mkuu kuanzisha baraza la taifa lauwezeshaji ,idara ya ushiriki wa watanzania katika uwekezaji ,aidha kupitia baraza hilo ilitoa majukumu mbalimbali ikiwemo kutathimini ushiriki wa watanzania katika sekta zote ‘’Alisema Katibu Mkuu DKT. Hamisi Mwinyimvua .

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Dkt. Mwinyimvua alisema kuwa katika zoezi hilo lakuratibu ushiriki wa watanzania katika uwekezaji katika sekta mbalimbali ,pia serikali itaipitia mikataba yakimataifa inayohusiana nauwekezaji mkubwa wandani .

Alisema kuwa kupitia Baraza la uwekezaji litahakikisha kuwa Tanzania inaongeza thamani ya uchumi wake kupitia sekta mbalimbali ikiwemo sekta yagesi asilia lengo nikuhakikisha taifa nawatazania kwa ujumla wanaufaika na uwekezaji wa hapa nchini .

‘’ilikuweza kufanikisha zoezi hili serikali imeandaa kongamano la siku mbili litakalo washirikisha wadau mbalimbali wa ndani nanje yanchi ili kuweza kushauriana nakujadili masuala mbalimbali yauwekezaji ili kuiwezesha serikali kuweka mipango madhubuti ya ushikirikishwaji wa watanzania kikamilifu ‘’Aliongeza Katibu Mkuu Mwinyimvua.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni