Jumanne, 30 Agosti 2016

TRL YATOA AUHENI YA NAULI KWA WAKAAZI WA DAR ES SALAAM.

Tokeo la picha la trl tanzania

BAADHI YA MABEHEWA YA SHIRIKA LA RELI YANAYO TUMIKA KATIKA USAFIRI KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM.



Timothy Marko.
KATIKA  kuhakikisha sekta ya usafirishaji inaimarika shirika la reli nchini (TRL) imetoa nauli  elekezi ya shilingi 600 kwa wasafiri wanaotumia  usafiri wa reli kwa wakaazi jiji la Dar es salaam.

Akizungumza na waandishi wahabari jijini Dar es salaam Kaimu Mkurugenzi wa shirilika hilo Nghwani Mdema amesema kuwa nauli hiyo elekezi ya shilingi 600 itaanza kutozwa baada ya wiki mbili kuanzia leo .

‘’Nauli hii itaendana sambamba na ile ya wanafunzi 100 baada ya mamlaka ya usafirishaji majini nan chi kavu kufanya ukokotozi juu ya gharama ya nauli ya usafiri huu ‘’Alisema Kaimu Mkurugenzi Ngwani  Mdema .

Kaimu Mkurugenzi Mdema alisema kuwa katika kuboresha huduma ya shirika la Reli shirika hilo linatarajia kuongeza mabehewa mawili ambapo hapo awali shirika hilo lilikuwa likitumia mahewa kumi nane na kufikikia mabehewa ishirini.

Alisema wa  agosti 9 mwaka huu waziri wa ujenzi ,uchukuzi na mawasiliano Profesa Makame Mbarawa alizindua safari za kutoka katikatikati ya jiji la Dar es salaam kwenda pugu huku shirika hilo likiwa na mabehewa 15 yanayotumika kusafirisha abiria .

‘’Kwa kipindi cha wiki moja shilika hili likuwa likitoa huduma kwa wananchi na wakaazi wa Dar es salaam awamu mbili asubuhi na jioni bila kutoza malipo yeyote’’Aliongeza Mdema .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni