Jumatano, 17 Agosti 2016

NDALICHAKO ATOA SIKU SABA KUHAKIKI WANAFUNZI HEWA WA ELIMU YA JUU

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Joyce Ndalichako akizungumza na waandishi habari kuhusu sakata la wanafunzi hewa Jijini Dar es Salaam
Timothy Marko

Kufuatia kuwepo kwa sintofahamu ya malipo hewa kwa wanafunzi wa elimu ya juu nchini, Serikali imewataka wakuu wa vyuo vikuu hapa nchini kuhakikisha wanafunzi waliochukua mikopo hiyo ambao hawakuwa na sifa stahiki kufanya marejesho ya mikopo hiyobaada ya siku saba.

Akizungumza na wahandishi wa Habari jijini Dar es Salaam Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amesema kuwa vyuo vya elimu vinatakiwa kuweka mfumo mzuri wa kuhifadhi kumbukumbu za wanafunzi kuanzia usajili na matokeo ya majaribio ya mitihani sambamba na akaunti  za benki ambazo mikopo hiyo ililipwa.

“Bodi ya Mikopo inapaswa kuchambua na kuingiza mara mabadiliko ya taarifa za wanafunzi kama ilivyo pelekwa kutoka vyuoni ili kuepusha ulipaji wa fedha kwa wanafunzi wasio stahili, hatua kali za kinidhamu zichukuliwe kwa wotevwaliohusika kufaniksha malipo kwa wanafunzi ambao hawapo vyuoni” Alisema Ndalichako

Waziri Ndalichako amesema ukaguzi huo utahusisha wafanyakazi wa bodi ya mikopo na vyuo husika pia amevitaka vyuo viweke utaratibu mzuri wa kudhibiti malipo kwa wanufaika wa mikopo ili kuepuka kufanya malipo ya wanafunzi hewa.

Pia Waziri Ndalichako ameeleza kuwa Wakuu wa vyuo waweke mifumo ya uhakiki wa  usahili wa matokeo ya wanafunzi yanayotumwa bodi ya mikopo, ambapo amesisitiza kuwa bodi ya mikopo watawajibika kwa usahili wa zoezi hilo kwani hivi karibuni kumebaini ka kuwepo kwa udanganyifu wa matokeo ya wanafunzi ambao hawakufnaya mtihani na wamefeli na wameandikiwa kuwa wamefaulu (PASS) ili waendelee kupata mikopo hiyo.


“Uchunguzi zaidi utafanyika kwa miaka iliyopita ili kubaini fedha za mikopo ambazo zimelipwa kwa watu wasio stahili hatua hii inatokana na matokeo ya uchunguzi ambao umebaini kuwepo kwa bbadhi ya wanafunzi waliohitimu tangu mwaka 2013 lakini wameendelea kupokea fedha na wengine wamefukuzwa kwa kushindwa masomo tangu mwaka 2013-2014 lakini bado wameendelea kulipwa hadi mwaka 2015-2016”.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni