Timothy
Marko .
KATIKA
kuhakikisha ajali za barabarani zinatokomezwa nchini ,Serikali imesema kuwa haitosita
kuwachukulia hatua madereva watakao kiuka sheria za barabarani ikiwemo
kuwapeleka mahakamani na kuwafungulia mashitaka .
Akizungumza
na waandishi wa habari mapema hii leo jijini Dar es salaam Naibu Waziri wa Mambo
ya Ndani Hamad Masauni amesema kuwa madereva wanaoendesha boda boda watakao
kiuka sheria za barabarani ikiwemo kupandisha abiria zaidi ya wawili maarufu
mshikaki jeshi la polisi litachukua hatua ya kumkamata mtuhumiwa huyo nakuweza
kumpeleka Mahabusu.
‘’kumekuwa
natabia ya madereva wa boda boda wamekuwa na tabia ya kubeba mshikaki tumeweka
sheria kali ikiwemo kuwafungulia mashitaka nakuwapeleka mahabusu nakisha
mahakamani ‘’Alisema Naibu Waziri Masauni Masauni .
Masauni
alisema kuwa sambamba nakutoa adhabu kwa madereva wa boda boda pia jeshi
la polisi halitosita kuwachukulia hatua za kinidhamu kwa mabasi ya abiria ambao
abiria wake hawafungi mkanda .
Alisema
Katika suala hilo jeshi la polisi halitomchukulia hatua za kisheria dereva
pekeyake bali hata abiria ambaye atakaye onekana hajafunga mkanda .
‘’Sambamba
na sheria hizi ,jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani tutaendelea kutoa
elimu ya usalama barabarani ikiwemo kuonesha maeneo yote tete yanayosababisha
ajali kwa kushirikiana na Tan roads’’Aliongeza Masauni .
Aliongeza
kuwa jeshi la polisi litaendelea kuwa chukulia hatua wale wote waliokuwa natabia
yakuweka vioo vilivyotiwa giza (tinted)ilikuweza kupunguza tatizo hilo la ajali .
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni