Jumanne, 19 Julai 2016

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU VILAINISHI VINAVYOTUMIWA ''MASHOGA".

Waziri  wa Afya Maendeleo ya jamii, Jinsia,wazee na  watoto Ummy Mwalimu
Timothy Marko.
Wizara ya Afya Maendeo ya Jamii jinsia Wazee na Watoto imepiga marufuku matumizi ya vilainishi vinavyotumiwa na baadhi ya makundi yanayojiuhusisha mapenzi ya jinsia moja.

Akizungumza na  waandishi wa habari jijini Dar es salaam jana Waziri  wa Afya Maendeleo ya jamii, Jinsia,wazee na  watoto Ummy Mwalimu alisema  vitendo vya mapenzi ya jinsia moja ni kinyume na  sheria  zilizoweka nchini na pia avitambuliki kabisa.

Alisema  serikali imeamua kuzuia vilainishi hivyo ambavyo  vimekuwa vikitumiwa na baadhi ya makundi  yanayojiusisha na mapenzi ya jinsia moja ili kupunguza ongezeko la maambukizi ya VVU.

“Kipaumbele cha  serikali hii ni kujenga wodi  za akinamama,kununulia vifaa vya kujifungulia pamoja na  ununua madawa hospitalini na  sio kutoa fedha kwa ajili ya vilainishi kwa makundi hayo”alisema.

Ummy alisema kuwa vitendo hivyo ni kinyume na maadili ya kitanzania pia serikali haitambui vitendo hivyo ambavyo vimekuwa ni kinyume na dini  zote nchini.

Alisema makundi hayo yapo hatarini kwa kiasi kikubwa kupata maambukizi mapya ya VVU kutokana na kujijusisha na vitendo hivyo  kwa kasi  zaidi.
Ummy alisema kuwa takwimu zilizopo zinaonbesha kuwa  mkoa  wa Dar es salaam pamoja na Dodoma imekuwa ikiongoza vitendo hivyo yvya mapenzi ya jinsia moja.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni