Ijumaa, 8 Aprili 2016

MUHONGO AWALILIA VIJANA WALIOKUWA NAUJUZI .

Tokeo la picha la waziri sospeter muhongo

waziri wanishati na madini Sospeter Muhongo

Timothy Marko .
WAZIRI  wanishati na madini Sospeter MUHONGO amewataka wafanyakazi  wa wizara yanishati na madini kufanya majadiliano nashilika la umeme latanesco kuweza kuongeza vyanzo vyauzalishaji umeme ili kuweza kufikia malengo ya uchumi wakati .

Akizungumza katika kikao chawafanyakazi katika wizara yake jijini Dar es salaam WAZIRI muhongo amewataka wafanyakazi wa wizara hiyo kuangalia namna yakuboresha miradi yaumeme ilkuweza kufikia megawati 1000 kwajili yakuendeleza  sekta yaviwanda .

''Nilazima mjadili vyanzo vya umeme vyanzo vingine vitapatikana wapi nilazima muangalie miradi yakusambaza umeme napia ninawaomba muweze kuangalia mikataba mibovu nakuondokana na rushwa ''Alisema WAZIRI Sospeter MUHONGO.

Waziri MUHONGO alisema kuwa nilazima wizarayake ifanye makusanyo yakodi itokanayo nasekta yamadini ilkuendeleza uchumi ilikuweza kufikia malengo yamilenia yamwaka 2025 yakuwa nchi yauchumi wakati .

alisema kuwa  nilazima kuwaachia nafasi wataalamu vijana waliokuwa naujuzi ikuweza kuleta ujuzimpya katika wizara nakuwawezesha vijana kushika nafasi za juu ilikuweza kuleta changamoto  yenye tija katika utendaji kazi .

''Nilazima tupandishe vyeo vya watumishi vijana wenye sifa kwa haraka ilikuweza kuleta ujuzi naufanisi katika utendaji wakazi ,ifike mahala wazee wasiwaonee wivu vijana wenye uwezo waweze kupandishwa vyeo ''Aliongeza Muhongo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni