Alhamisi, 14 Aprili 2016

ASILIMIA 71 WANANCHI WATANZANIA HAWAFANYI KAZI.

Tokeo la picha la ofisi ya takwimu tanzania

OFISI YA TAKWIMU



Timothy Marko.
WAKATI Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Jonh Pombe Magufuli akihimiza watanzania kufanya kazi imebainika asilimia 71ya watanzania hawafanyi kazi za uzalishaji ili kujiletea maendeleo .

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na ofisi yatakwimu kupitia toleo la utafiti la mwaka 2014 lijulikanalo kama ‘’Intergrated Labour force Survey Analytical Report imeoneshakuwa zaidi ya watu walipo kati ya umri  wa miaka 15  nakuendelea wamekuwa wakitumia muda mwingi wa wastarehe ikiwemo kujihudumia nakulala kuliko kufanya kazi za uzalishaji mali .

‘’Uchambuzi wa kijinsia ulionesha kuwa  wanaume watumia muda wao mwingi katikashughuli za kiuchumi kwa asilimia 28 huku wanawake wakitumia asilimia 13 .5 kwashughuli za kiuchumi wakati huo huo wanawake walitumia muda mwingi washughuli za nyumbani zisizokuwa na malipo ikilinganishwa na wanaume asilimia 4.4 ‘’Ilisema ripoti hiyo.

Ripoti hiyo llibainishakuwa hali yaukosefu wa ajira kwawatu wenye ulemavu kati yaumri wamiaka 15 nakuenelea ni asilimia 12.4 ambapo ripoti hiyo ilidai kuwa kiwango hicho nikikubwa kuliko kiwango cha kitaifa cha asilimia 10.3 

Ilisema kuwa hali yawanawake wenye ulemavu ni asilimia 14.6 ikilinganishwa na asilimia 9.5ya wanaume wenye uwezo wakufanya kazi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni